الاثنين، 9 مارس 2015

55 - Surat Ar-Rahman, Medinan, 78 verses 55- سورة الرحمن, مدنية, 78 آية : Arabic and Swahili


55 - Surat Ar-Rahman, Medinan, 78 verses
55- سورة الرحمن, مدنية, 78 آية


Arabic

بِسمِ اللَّهِ الرَّحمٰنِ الرَّحيمِ
الرَّحمٰنُ ﴿١﴾ عَلَّمَ القُرءانَ ﴿٢﴾ خَلَقَ الإِنسٰنَ ﴿٣﴾ عَلَّمَهُ البَيانَ ﴿٤﴾ الشَّمسُ وَالقَمَرُ بِحُسبانٍ ﴿٥﴾ وَالنَّجمُ وَالشَّجَرُ يَسجُدانِ ﴿٦﴾ وَالسَّماءَ رَفَعَها وَوَضَعَ الميزانَ ﴿٧﴾ أَلّا تَطغَوا فِى الميزانِ ﴿٨﴾ وَأَقيمُوا الوَزنَ بِالقِسطِ وَلا تُخسِرُوا الميزانَ﴿٩﴾ وَالأَرضَ وَضَعَها لِلأَنامِ ﴿١٠﴾ فيها فٰكِهَةٌ وَالنَّخلُ ذاتُ الأَكمامِ ﴿١١﴾ وَالحَبُّ ذُو العَصفِ وَالرَّيحانُ ﴿١٢﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿١٣﴾ خَلَقَ الإِنسٰنَ مِن صَلصٰلٍ كَالفَخّارِ﴿١٤﴾ وَخَلَقَ الجانَّ مِن مارِجٍ مِن نارٍ ﴿١٥﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿١٦﴾ رَبُّ المَشرِقَينِ وَرَبُّ المَغرِبَينِ ﴿١٧﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿١٨﴾ مَرَجَ البَحرَينِ يَلتَقِيانِ ﴿١٩﴾بَينَهُما بَرزَخٌ لا يَبغِيانِ ﴿٢٠﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٢١﴾ يَخرُجُ مِنهُمَا اللُّؤلُؤُ وَالمَرجانُ ﴿٢٢﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٢٣﴾ وَلَهُ الجَوارِ المُنشَـٔاتُ فِى البَحرِ كَالأَعلٰمِ ﴿٢٤﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٢٥﴾ كُلُّ مَن عَلَيها فانٍ ﴿٢٦﴾ وَيَبقىٰ وَجهُ رَبِّكَ ذُو الجَلٰلِ وَالإِكرامِ ﴿٢٧﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٢٨﴾ يَسـَٔلُهُ مَن فِى السَّمٰوٰتِ وَالأَرضِ ۚ كُلَّ يَومٍ هُوَ فى شَأنٍ ﴿٢٩﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٣٠﴾ سَنَفرُغُ لَكُم أَيُّهَ الثَّقَلانِ ﴿٣١﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٣٢﴾ يٰمَعشَرَ الجِنِّ وَالإِنسِ إِنِ استَطَعتُم أَن تَنفُذوا مِن أَقطارِ السَّمٰوٰتِ وَالأَرضِ فَانفُذوا ۚ لا تَنفُذونَ إِلّا بِسُلطٰنٍ ﴿٣٣﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ﴿٣٤﴾ يُرسَلُ عَلَيكُما شُواظٌ مِن نارٍ وَنُحاسٌ فَلا تَنتَصِرانِ ﴿٣٥﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٣٦﴾ فَإِذَا انشَقَّتِ السَّماءُ فَكانَت وَردَةً كَالدِّهانِ ﴿٣٧﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٣٨﴾ فَيَومَئِذٍ لا يُسـَٔلُ عَن ذَنبِهِ إِنسٌ وَلا جانٌّ ﴿٣٩﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٤٠﴾ يُعرَفُ المُجرِمونَ بِسيمٰهُم فَيُؤخَذُ بِالنَّوٰصى وَالأَقدامِ ﴿٤١﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٤٢﴾ هٰذِهِ جَهَنَّمُ الَّتى يُكَذِّبُ بِهَا المُجرِمونَ﴿٤٣﴾ يَطوفونَ بَينَها وَبَينَ حَميمٍ ءانٍ ﴿٤٤﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٤٥﴾ وَلِمَن خافَ مَقامَ رَبِّهِ جَنَّتانِ ﴿٤٦﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٤٧﴾ ذَواتا أَفنانٍ ﴿٤٨﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٤٩﴾ فيهِما عَينانِ تَجرِيانِ ﴿٥٠﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٥١﴾ فيهِما مِن كُلِّ  فٰكِهَةٍ زَوجانِ ﴿٥٢﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٥٣﴾ مُتَّكِـٔينَ عَلىٰ فُرُشٍ بَطائِنُها مِن إِستَبرَقٍ ۚ وَجَنَى الجَنَّتَينِ دانٍ ﴿٥٤﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ﴿٥٥﴾  فيهِنَّ قٰصِرٰتُ الطَّرفِ لَم يَطمِثهُنَّ إِنسٌ قَبلَهُم وَلا جانٌّ ﴿٥٦﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٥٧﴾ كَأَنَّهُنَّ الياقوتُ وَالمَرجانُ ﴿٥٨﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٥٩﴾ هَل جَزاءُ الإِحسٰنِ إِلَّا الإِحسٰنُ ﴿٦٠﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٦١﴾ وَمِن دونِهِما جَنَّتانِ ﴿٦٢﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٦٣﴾ مُدهامَّتانِ ﴿٦٤﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٦٥﴾ فيهِما عَينانِ نَضّاخَتانِ ﴿٦٦﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٦٧﴾ فيهِما فٰكِهَةٌ وَنَخلٌ وَرُمّانٌ ﴿٦٨﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ﴿٦٩﴾ فيهِنَّ خَيرٰتٌ حِسانٌ ﴿٧٠﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٧١﴾ حورٌ مَقصورٰتٌ فِى الخِيامِ ﴿٧٢﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٧٣﴾ لَم يَطمِثهُنَّ إِنسٌ قَبلَهُم وَلا جانٌّ ﴿٧٤﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٧٥﴾ مُتَّكِـٔينَ عَلىٰ رَفرَفٍ خُضرٍ وَعَبقَرِىٍّ حِسانٍ ﴿٧٦﴾ فَبِأَىِّ ءالاءِ رَبِّكُما تُكَذِّبانِ ﴿٧٧﴾ تَبٰرَكَ اسمُ رَبِّكَ ذِى الجَلٰلِ وَالإِكرامِ ﴿٧٨﴾

 Swahili
 KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.


(1) Arrah'man, Mwingi wa Rehema (2) Amefundisha Qur'ani. (3) Amemuumba mwanaadamu, (4) Akamfundisha kubaini. (5) Jua na mwezi huenda kwa hisabu. (6) Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea. (7) Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,(8) Ili msidhulumu katika mizani. (9) Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.(10) Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe. (11) Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba. (12) Na nafaka zenye makapi, na rehani. (13) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha (14) Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo.. (15) Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto. (16) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha (17) Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili. (18) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (19) Anaziendesha bahari mbili zikutane; (20)Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane. (21) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (22) Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani. (23) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (24) Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima. (25) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (26)Kila kilioko juu yake kitatoweka. (27) Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu. (28) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (29)Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo. (30)Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (31) Tutakuhisabuni enyi makundi mawili. (32) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (33) Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa madaraka. (34) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (35)Mtapelekewa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda. (36) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (37) Itakapo pasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta.(38) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (39) Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini. (40) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?(41) Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu. (42) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (43) Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha. (44) Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka. (45) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (46) Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili. (47) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (48) Bustani zenye matawi yaliyo tanda. (49) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (50)Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita. (51) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (52) Humo katika kila matunda zimo namna mbili. (53) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (54) Wawe wameegemea matandiko yenye bit'ana ya hariri nzito; na matunda ya Bustani hizo yapo karibu. (55) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (56) Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini. (57) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (58) Kama kwamba wao ni yakuti na marijani. (59) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha. (60) Ati yaweza kuwa malipo ya ihsani ila ihsani? (61) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (62) Na zaidi ya hizo zipo Bustani nyengine mbili. (63) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (64) Za kijani kibivu.(65) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (66) Na chemchem mbili zinazo furika. (67) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (68) Imo humo miti ya matunda, na mitende na mikomamanga. (69) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (70) Humo wamo wanawake wema wazuri. (71) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (72) Wanawake wazuri wanao tawishwa katika makhema. (73) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (74)Hajawagusa mtu wala jini kabla yao. (75) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (76) Wameegemea juu ya matakia ya kijani na mazulia mazuri. (77) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha? (78) Limetukuka jina la Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.

ليست هناك تعليقات:

إرسال تعليق